
Rais
John Magufuli akisalimiana na Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua
Nassari aliyekuwa mmoja wa viongozi na wananchi waliojitokeza kwa wingi
kumpokea alipowasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA)
kwa ajili ya kuongoza mkutano wa 17 wa kawaida wa Wakuu wa Nchi za
Jumuiya ya Afrika Mashariki unaotarajiwa kufanyika jijini Arusha. (Picha
na Ikulu).
Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), Rais Magufuli alilakiwa na viongozi wa serikali, vyama vya siasa pamoja na vikundi vya burudani za ngoma kabla ya kuelekea Arusha Mjini.
Rais Magufuli ndiye Mwenyekiti wa sasa wa Jumuiya ya Afrika Mashariki inayojumuisha nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi.
Kabla ya kuongoza kikao hicho, Rais Magufuli anatarajiwa kukutana na kufanya mazungumzo ya ana kwa ana na viongozi wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Alhamisi wiki hii, Magufuli na Rais wa Kenya, wataweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa barabara ya Arusha - Holili - Taveta - Voi inayounganisha Tanzania na Kenya.
Barabara hiyo ni sehemu ya miradi ya maendeleo ya Jumuiya ya Afrika Mashariki inayotekelezwa na nchi wanachama wa jumuiya hiyo.
No comments:
Post a Comment